Thursday, April 16, 2015

>>> >>> >>>

ABEID KARUME NA EDWARD SOKOINE, MASHUJAA WA TAIFA WALIOFARIKI MWEZI APRILI

Imechapwa na: UV MAPINDUZI - 6:29 AM

Na Comrad Bambino .
Kila ifikapo mwezi wa nne taifa huzizima kwa masikitiko na majonzi likiwakumbuka mashujaa wake wawili Ndugu Abeid Karume mwasisi mpambanaji na kiongozi wa mapinduzi ya wengi visiwani Zanzibar ambayo ndiyo yalileta uhuru wa kweli kwa waafrika wazanzabari na Ndugu Edward Sokoine aliyekuwa waziri mkuu wa Jamhuri ya muungano Tanzania mwaka 1977 hadi 1980 kishakurudi tena ofisini mwaka 1983 hadi mwaka 1984.
Hawa walikuwa viongozi mashujaa kabisa katika historia ya kuleta maendeleo katika nchi yetu. Tukianza na Ndugu Abeid Karume aliyekuwa raisi wa kwanza wa Zanzibar kiongozi wa mapinduzi yaliyoleta ukombozi wa wengi visiwani Zanzibar. Abeid Karume atakumbukwa kwa mengi visiwani Zanzibar na Tanzania kwa ujumla.

Hayati Edward Sokoine naye atakumbukwa kwa mengi kama mzalendo mpigania maendeleo Tanzania, ni kweli isiyofichika kuwa hayati Sokoine alikuwa waziri mkuu wa Tanzania aliyekuwa na ndoto kubwa ya maendeleo ya taifa letu. Akiwa mzalendo aliye bobea katika siasa za usawa wa kibinadamu na ujamaa hayati Sokoine alionekana kama nuru ya maendeleo ya taifa letu.

Kwenye picha ya kulia ni baba wa taifa Mwl. Julius K. Nyerere akimsikiliza kwa umakini hayati Edward M. Sokoine katika moja ya majukumu ya kimaendeleo aliyokuwa akiyasimamia, Chini kushoto ni waasisi wa taifa letu hayati baba wa taifa Mwl. Julius K Nyerere na hayati kiongozi wa mapinduzi Zanzibar Abeid Karume katika moja ya majukumu muhimu ya taifa letu.




Kweli Chema hakidumu! Leo hatupo nao tena wazalendo waleta maendeleo ya taifa letu wametutoka wapambanaji hawa waliokuwa nuru ya maendeleo ya taifa letu. Tuzidi kuwaombea wazalendo hawa na wazalendo wengine wote wa taifa letu wapumzike mahala pema peponi Ameni!.

Shirikisha

& Hoji

0 comments:

Post a Comment

Download It from Here

MonotataPx I Mbinotrix I MonotataPx I Mbinotrix