Na Mwandishi Wetu
Jumuiya
ya wazazi chama cha mapinduzi una adhimisha miaka 60 tangu kuanzishwa kwake,
wiki ya wazazi CCM ime adhimishwa rasmi mkoani Mbeya kitaifa. Akipokea taarifa
ya Mkoa Mbeya mara baada ya kuwasili mkoani hapo Mwenyekiti wa jumuiya ya
wazazi taifa Ndugu Alhaj Abdallah Bulembo alizungumzia suala la mbio za kuwania
nafasi ya kugombea uraisi ndani ya chama na kutoa msimamo wa jumuiya ya wazazi.
Alisema kuwa wapo baadhi ya wawania nafasi hiyo ya kupeperusha bendera ya chama
Oktoba walioanza kueneza uvumi kuwa jumuiya hiyo inawaunga mkono katika
harakati zao za kutafuta uungwaji mkono, jambo ambalo si la kweli.
“Jumuiya
ya wazazi itamuunga mkono mgombea wa CCM aliyepitishwa na chama kupitia vikao
halali, wale wanaodhani kuwa wanaweza kuitumia jumuiya hii kama ngazi ya
kufanikisha malengo yao watambue kuwa hilo haliwezekani” alisisitiza Ndugu
Bulembo
Pia
Ndugu Bulembo alizidi kusisitiza kuwa
jumuiya ya wazazi inakutana mjini mbeya ili kuadhimisha wiki ya jumuiya hiyo,
kutafakari sera ya maadili na wala si kwenda kumpigia debe mtu yeyote ndani au
nje ya chama. Hata hivyo hakukataza wanachama wa jumuiya hiyo kumuunga mkono
mtu yeyote ndani ya chama kwani hilo
litakuwa ni swala la mtu binafsi wala
siyo jumuiya.
Awali
akisoma taarifa ya chama mkoa wa mbeya katibu wa chama mkoa alisema kuwa
kitendo cha jumuiya hiyo kufanya maadhimisho hayo mkoani Mbeya ni sawa na
kuandika historia kwa mkoa huo kwani
taifa linataraji kukutana na matukio mawili makubwa ambayo ni kupatikana
kwa katiba mpya pamoja na uchaguzi mkuu wa madiwani, wabunge na raisi.


0 comments:
Post a Comment