Monday, January 16, 2017

>>>

UKAME WA TANZANIA UNAOTESHA BANGI, UNAKAUSHA MAHINDI NA MTAMA

Imechapwa na: UV MAPINDUZI - 10:48 AM

Na Menuka Jr.

Mambo yanayoendelea katika Nchi hii yanaweza kukusukuma kucheka hata pale isipohitajika๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚
Hivi utajiskiaje kusikia kuwa katika Nchi moja yenye Ukame Bangi zinazooteshwa na Wapinzani zinastawi wakati huohuo Chakula kinachooyeshwa na Wananchi kinakauka?

Ni Wiki mbili sasa Wanasiasa wa Nchi yetu hasa Wapinzani (ACT-Wazalendo, CHADEMA), wameamua kujitoa fahamu kabisa ilimradi tu watimize matakwa yao kisiasa.Ni bahati mbaya sana kuwa Wanasiasa wetu ni wasahaulifu mno! Wastani wao wa kusahau ni kilomita tatu kwa saa yaani 3km/hr. Na kadiri muda unavyokwenda ndivyo hali inakua mbaya zaidi.

Kwa usahaulifu wao wanadhani Watanzania wote ni mifano yao, kwamba hatuna kumbukumbu kwa matendo na taarifa za Nchi yetu. Wameliwa! Kama unataka kunielewa vizuri kabisa, usipate taabu, tufuatane katika tafakari hii.

Mwishoni mwa Mwaka jana huko Arusha alikamatwa Diwani wa Kata ya Lemanyata Losyeku Kilusu (CHADEMA),Wenyeviti Saba wa Vitongoji (CHADEMA) na Wenyeviti Watatu wa Vijiji (CHADEMA). Viongozi wote hawa wanaotokana na  Chama cha Demokrasia na Maendeleo ya Njaa na Ukame Bandia walikamatwa baada ya kubainika kuwa wanamiliki na kuendesha kilimo cha Bangi kwa Shamba lenye ukubwa zaidi ya Hekali Nane.  Ikumbukwe kuwa Kilimo cha Bangi ni haramu kwa Sheria za Nchi yetu.

Ukiitazama vizuri picha ya Shamba hilo la Bangi lilivyonawili na kustawi kwa rangi ya kijani kibichi huwezi kukwepa kuhitimisha kuwa Ardhi ya Tanzania ni kiboko, ina rutuba ya kutosha na maji ya kustawisha Mimea na Mazao.

Baada ya muda mfupi kupita, Viongozi hao walima Bangi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo ya Njaa na Ukame Bandia, wameibuka na taarifa ya Njaa Nchini na Ukame wa hali ya juu. Wanasema kuwa, hali ya Chakula Nchini ni mbaya mno kwa sababu hakuna Mvua na Mifugo inakufa kwa kukosa Nyasi na Maji. Watu hawa kwa nia ovu kabisa, wamediriki kutumia picha za Nchi kama Sudani na Afrika Kusini kutaka kuwaaminisha Watu wa Nchi hii kuwa kuna ukame. Haya ni mambo makubwa mno katika Nchi.

Baada ya mambo haya pamoja na juhudi kubwa za kulifarakanisha Taifa hili kwa kisingizio cha njaa, mimi nimejifunza mambo kadhaa kama ifuatavyo;

Mosi, Ni Tanzania pekee ambapo Ukame unaotesha zaidi Bangi kuliko Mazao ya Chakula ndio maana  Bangi Hekali mbili zinaweza kunawili na kustawi, lkn Mahindi na Mtama vikakauka kau.

Pili, Viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo ya Njaa na Ukame wanaweza kulima kwa ustadi Bangi haramu lkn hawawezi kabisa kulima ama kuwashauli na kuwaongoza Watanzania ktk kulima mazao ya Chakula.

Tatu, Ni Tanzania pekee ambapo Ukame hutokea kama shoti ya Umeme bila ishara na ghafra mifugo mamia kwa mamia kufariki na Mahindi kukauka huku picha zinazotumiwa zikiazimwa kutoka South Sudan na South Afrika. Tunahitaji Maombo maalum kwa Wapinzani wa Nchi hii.

Nne, Ni Tanzania pekee ambapo taarifa za Baa(Janga) la Njaa hazitokani na utafiti wala takwimu isipokuwa Chaguzi ndogo za Madiwani kama Kijichi, Geita na huko Arusha kwa ajili ya maslahi ya Kisiasa.

Tano, Ni Tanzania pekee ambapo Janga kubwa kama linahubiriwa kisiasa kwa kuwashawishi Wananchi wasifanye kazi kwa ajili ya Uzalishaji mali bali walalame kwa Rais na kuingoja Serikali kutatua matatizo yao.

Kwakweli tunahitaji akili kubwa mno kuishi na Watu wa namna hii. Wanasiasa Wachonganishi kama Zitto Kabwe na Lowassa ni hatari mno kwa Ustawi wa Taifa letu. Hakuna Nchi ambayo imewahi kuendelea ama kutatua Matatizo yanayowakabili kwa kuendekeza maneno bila kufanya kazi. Ni lazima tufanye kazi kwa Maendeleo ya Nchi yetu.

#NamuungaMkonoRaisWangu

#NafanyaKaziKwaMaendeleoYaNchiYangu.

Shirikisha

& Hoji

0 comments:

Post a Comment

Download It from Here

MonotataPx I Mbinotrix I MonotataPx I Mbinotrix